January 13, 2026

WatuCrash

📚 Education & Learning Hub (Primary + Secondary)

ca-app-pub-5779332594648854/1423561520
Kiswahili

KISWAHILI DARASA LA TANO

nukuu za mtaala mpya

1SURA YA KWANZA

1.0 KUWASILIANA KATIKA MIKTADHA MBALIMBALI

1.1 Kuendeleza mazungumzo katika miktadha mbalimbali

a) Kutumia msamiati katika kusimulia matukio, habari na vitu mbalimbali

kwa kujiamini

KUSIMULIA MATUKIO

Nini maana ya msamiati?

Ni mkusanyiko wa maneno yanayotumiwa katika lugha fulani ili kufikisha

maana au mawazo

Kwa kifupi, msamiati ni hazina ya maneno ya lugha

Mfano wa misamiati na maana zake

1. Katili – kutokuwa na huruma

2. Mwambao – sehemu ya nchi iliyokaribu na bahari

3. Ghala – jengo la kuhifadhia vitu au bodhaa

4. Kiuka – fanya isivyostahili

5. Dafina – vitu vya thamani vilivyofichwa katika ardhi

6. Shubiri – kitu chenye uchungu sana

7. Shangazi – dada wa baba

8. Bikira – mwanamke au msichana ambaye hajawahi kushiriki tendo la

ndoa

9. Jabali – mwamba mkubwa pia hutumika kumaanisha mtu mwenye nguvu

na jasiri

10. Hitilafiana – kutoafikiana katika kufanya mambo mbalimbali

11. Wahaini – watu ambao wapo tayari kuidhuru nchi yao

12. Fukara – mtu maskini au mwenye uwezo mdogo wa kiuchumi

13. Samba – enea kila mahali

14. Kongwe – kilicho cha zamani sana

15. Utepe – Kamba laini mara nyingi ya mapambo

16. Mvinyo – kinywaji cha kienyeji cha kilevi chenye chachu ya zabibu

17. Uhaba – ukosefu wa kutosha wa kitu

18. Mwangaza – nuru au mwanga unaoruhusu kuona vizuri

19. Takrima – upendo au zawadi inayotolewa kwa heshima au ukarimu

20. Dhahiri – bila ya kuficha

21. Ujasiri – uwezo wa kukabiliana na hatari au hofu

222. Hodari – mtu mwenye ujuzi au uwezo mkubwa

23. Ushirikiano – kufanya kazi Pamoja kwa lengo moja

24. Ustadi – uwezo wa kufanya jambo vizuri au kwa ujuzi

25. Ubora – kiwango cha juu au cha thamani

26. Mwongozo – maelekezo au kielelezo kinachosaidia kufanya jambo

27. Dhihaka – mchezo wa kejeli kwa kumdharau mtu

28. Hila – njia au mbinu ya udanganyifu, ujanja wenye nia mbaya au ulaghai

Soma hadithi ifuatayo kisha jibu maswali yanayofuata

Mtengo wa vitendawili

Nzige, Panya na Kiwavi waliishi msituni Pamoja na Kipepeo, Nyoka, Ndege,

Mjusi na Mzee Ngedere. Nzige, Panya na Kiwavi walikuwa marafiki

walioshirikiana kwa mambo mabaya. Mara nyingi marafiki hawa walivamia

mashamba ya Binadamu na kufanya uharibifu wa mazao.Walileta kero kubwa

Binadamu alitumia mbinu nyingi ili kuwaangamiza viumbe hao lakini mbinu

zake hazikufua dafu.Siku moja, Mzee Ngedere alikwenda kwa Binadamu

kuomba kazi ya kuwaangamiza Nzige, Panya na Kiwavi

Binadamu alicheka sana kwa kumdharau Mzee Ngedere.Mzee Ngedere

akasema “Usinichekeshe “. Binadamu akamjibu , “Mimi nimehagaika miaka

nenda miaka rudi sijaweza kuwakamata, wewe utawezaje na uzee wako,”

Mzee Ngedere alieleza

“Utahitaji malipo gani? “ Binadamu aliuliza.Mze Ngedere akamjibu kuwa

atajilipa kwa kuchukua mazao anayoyataka shambani kwa binadamu.

Binadamu alimruhusu Mzee Ngedere. Mzee Ngedere akaandaa tangazo kuwa

kutakuwa na shindano la kutegua vitendawili.A liahidi zawadi ya shamba na

ghala la chakula kizuri kwa atakayetegua kitendawili chake kwa usahihi

Nzige, Panya na Kiwavi walilipata tangazo hilo wakiwa wamejibanza

mafichoni. Nzige akawauliza wenzake, “Rafiki zangu, hivi mnaujua utamu wa

vitendawili? “Kiwavi akajibu, “Mimi ninajua >Vitendawili ni vitamu kuliko

hata chakula.Twendeni nikawaoneshe uhodari wangu wa kutegua vitendawili.”

Panya naye hakuwa nyuma. Akasema , “Hilo shamba na ghala lazima nivipate

mimi.

3Nitafaidi utamu wa vitendawili na nitajipatia ghala la vyakula vizuri. Lazima

nife kishujaa kupta ushindi huu.”

“Hebu tusiandikie mate na wino ungalipo. Twendeni tukashindane.”Kiwavi

aliwahimiza wenzake. Wote wakachapa mguu kuelekea jukwaa la kufanyia

shindano. Wanyama na wadudu wengine walipowaona Panya na wenzake

wakiingia ukumbini kwa maringo, Waliwashangilia kwa nguvu.Nzige, Panya na

Kiwavi wakajipanga nyuma na kuwa wa mwishomwisho ili vitendawili vigumu

zaidi viishe

Kipepeo, Nyoka, Ndege na Mjusi ndo waliotangulia .Wote wakashindwa

kutegua vitendawili vya mzee Ngedere. Nzige, Panya na Kiwavi hawakuacha

nyuma maringo yao ikiwa ni moja ya silaha ya ushindi wao.Hatimaye ,

ikawadia zamu ya Kiwavi. Alijinyonganyonga kwa madaha akapanda jukwaani

na kusubiri kitendawili .

“Kitendawili”Mzee Ngedere alisema. Kiwavi akajibu “Tega.”

“Nikikutanana na adui yangu nanyong’onyea.Nipatie jib una maana yake.”Mzee

ngedere alitega na kuomba jibu `Kiwavi alichemsha bongo akajibu haraka bila

kupoteza muda, “Jiubu lake ugonjwa.Maana yake ni kuwa ugonjwa

umefananishwa na adui, ugonjwa ni adui mkubwa wa viumbe.Binadamu

akikutana na ugonjwa, anakuwa mnyonge. Hata sisi viumbe wengine vivyo

hivyo.” Mzee Ngedere akamwambia, “Umepata!”

Panya alisogea akarukaruka kwa mikogo jukwaani. Mzee Ngedere akamtegea

kitendawili chake, “Adui tumemzingira lakini hatumuwezi.”Panya akajibu

“jibu lake ni moto.Maana yake ni kuwa hata tukiwa wengi kiasi gani hatuwezi

kukabiliana na joto la moto tunaouoata.Moto umefananishwa na adui ambaye

watu wamemzunguka kana kwamba wanamshabulia, “Mzee Ngedere

akamwambia, “Umepata

Baada ya panya kutegua kitendawili, Nzige akawa wa mwisho kutegua

kitendawili chake.Mzee Ndegere akatega akisema, “Ukumbuu wa babu

mrefu.”Nzige aliyainua mabawa yake kwa mbwembwe na kutoa sauti y anti nti

nti! Kisha akajibu, “Njia! Maana yake ni kwamba njia ni ndefu kama ukumbuu.

Kitendawili hiki kinafananisha urefu wa njia na mshipi.”

Mzee Ngedere aliwapongeza marafiki hao watatu kwa kutegua vitendawili na

kuvipatia maana zake kwa usahihi.Akawaomba waende kwenye chumba cha

mapumziko ili wasubiri hatua ya pili .Waliingia kwenye chumba mlimokuwa na

chakula kizuri kilichoandaliwa na mzee Ngeder.Wakaanza kula. Siku za mwizi

ni arobaini, na ujanja mwingi mbele kiza. Walipogutuka wakajikuta

4wamekwishafungiwa humo, huku nje binadamu akiwatizama kwa dhihaka.

Wakadhani ni kiinimacho. Kumbe mzee Ngedere alikuwa amekula njama

kuwakamata kwa hila na hilo lilikuwa gereza la waharibifu wa mazao

Binadamu alimshukuru Mzee Ngedere kwa msaada wake akisema , “Ama kweli

umadhaniaye ndiye kumbe siye! Mze Ngedere naye alimshukuru Binadamu

kwa kumpatia nafasi, kisha akarejea mlimani.Kama malipo ya kazi hiyo, Mzee

Ngedere Ngedere wakati mwingine huenda kwenye mashamba ya binadamu na

kula mazao

Zoezi 01 ufahamu

Eleza kwa ufupi matukio yaliyotokea katika hadithi uliyoisoma

Umejifunza nini kutokana na hadithi hii?

Binadamu alijaribu kuwaangamiza Panya na wenzake kwa muda gani

bila mafanikio?

4. Taja zawadi mbili amabazo Mzee Ngedere aliahidi kumpa mshindi wa

kutegua vitendawili

5. Nani aliyewambia wenzake wasiandikie mate na wino ungalipo?

BACK TO SCHOOL ONLINE MATERIAL

Karibu ujipatie

1. 2. 3. 1.scheme of work| – azimio la kazi

2.Lesson plan – Andalio la somo

3.Lesson Notes – Nukuu za somo

4.Log Book – Shajara

5.Holiday Package

Karibu kwa huduma nzuri uaminifu na uhakika Zaidi

Piga 0694361925 WhatsApp 0627064154

5

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *