January 13, 2026

WatuCrash

📚 Education & Learning Hub (Primary + Secondary)

ca-app-pub-5779332594648854/1423561520
science

Nukuu za somo la sayansi darasa la Tano

NUKUU ZA SAYANSI MTAALA MPYA

Nukuu za mtaala mpya

DARASA LA TANO

2026

SURA YA KWANZA

MFUMO WA MMENG’ENYO WA CHAKULA

Dhana ya mfumo wa mmenge’nyo wa chakula

1Mmeng’enyo wa chakula ni mchakato wa kibailojia ambapo chakula

huvunjwavunjwa kuwa chembechembe ndogo zenye virutubisho ambavyo

mwili unaweza kufyonza.

Mmeng’enyo wa chakula hufanyika katika mfumo wa mmeng’enyo wa chakula

Mfumo wa mmeng’enyo wa chakula ni mkusanyiko wa ogani au viungo vya

mwili wa binadamu vinavyohusika na kuvunjavunja chakula kuwa

chembechembe ndogo zenye virutubisho zinazoweza kufyonzwa na kutumiwa

na mwili

Ili kudumisha afya ya mfumo huu, ni muhimu kula mlo kamili kwa wakati

sahihi, kunywa maji ya kutosha, kuepuka kula vyakula vyenye mafuta au sukari

kwa wingi ili kuimarisha afya ya mfumo wa mmeng’enyo wa chakula

Mbali na binadamu, wanyama wengine pia wana mifumo ya kumeng’enya

chakula inayotofautiana kutokana na aina ya vyakula wanavyokula

Sehemu za mfumo wa mmeng’enyo wa chakula

Mfumo wa mmeng’enyo wa chakula unahusisha ogani mbalimbali ambazo

hufanya kazi kwa Pamoja ili kurahisisha uvunjwaji wa chakula. Mfumo wa

mmeng’enyo wa chakula wa binadamu huanzia kwenye kinywa hadi kwenye

njia ya haja kubwa. Mfumo huu unajumuisha njia ya chakula, ogani na tezi

zinazofanya kazi Pamoja

Sehemu kuu za njia ya chakula ni

a. Kinywa

b. Koromeo

c. Umio

d. Mfuko wat umbo

e. Utumbo mwembamba

f. Utumbo mpana

Utumbo mwembamba unajumuisha duodeni na iliamu. Vilevile, utumbo mpana

unajumuisha koloni, puru na njia ya kutolea haja kubwa

Mfumo wa mmeng’enyo wa chakula pia unajumuisha tezi za mate na zile

zinazopatikana katika mfuko wat umbo. Vilevile, baadhi ya ogani kama ini,

2kongosho na kibofu nyongo zina tezi zinazozalisha vimeng’enya vinavyotumika

katika kumeng’enya chakula

Kinywa

Ni sehemu ya kwanza ambapo chakula huingia. Hapa chakula hutafunwa na

kuchanganywa na mate ili kirahisishe kumezwa na kuanza kumeng’enywa.

Koromeo

Ni njia ya kupitishia chakula kutoka kinywa kwenda umio. Husaidia kuelekeza

chakula kisiingie kwenye njia ya hewa.

Umio

Ni mrija unaosafirisha chakula kutoka koromeo hadi mfuko wat umbo kwa

kutumia misuli inayojikaza na kulegea.

Mfuko wa tumbo

Hapa chakula huchanganywa na aside na vimeng’enya ili kivunjwe vipande

vidogo na kuwa uji laini.

3Utumbo mwembamba

Ndiyo sehemu kuu ya mmeng’enyo na ufyonzwaji wa virutubisho kama sukari,

protini na mafuta kwenda kwenye damu.

Utumbo mpana

Husaidia kufyonza maji na madini yaliyokusanya na kukaza kinyesi kabla ya

kuelekezwa kwenye puru.

Koloni

Ni sehemu ya utumbo mpana inayokusanya na kukaza kinyesi kabla ya

kuelekezwa kwenye puru.

Puru

Ni sehemu ya kuhifadhia kinyesi kwa muda mfupi kabla ya kutolewa nje ya

mwili.

Njia ya kutolea haja kubwa

Ni tundu la mwisho ambapo kinyesi hutolewa nje ya mwili.Kinyesi ni mabaki

ya chakula ambayo hayakumeng’enywa na kufyonzwa na mfumo wa

mmeng’enyo wa chakula

Kasoro katika mfumo wa mmeng’enyo wa chakula

kasoro katika mfumo wa mmeng’enyo wa chakula ni hali inayoathiri utendaji

wa kazi wa kawaida wa mfumo wa mmeng’enyo wa chakula na kufanya iwe

vigumu kwa mwili kumudu kumeng’enya na kufyonza chakula ipasavyo.

Kasoro hizo zinaweza kuwa za kimaumbile, kurithi au zinazotokana na mtindo

wa Maisha na lishe duni. Baadhi ya kasoro za mfumo wa mmeng’enyo wa

chakula ni kama zifuatazo

1. Kupata choo kigumu

Ni hali ambayo kinyesi huwa kigumu sana na kikavu kasoro hii husababishwa

na ulaji wa vyakula vyenye kiwango cha chini cha nyuzinyuzi, kutokunywa

maji ya kutosha na ukosefu wa mazoezi ya mwili.Pia, matatizo ya kiafya kama

vile utendaji duni wa utumbo mpana husababisha kupata choo kigumu

Njia za kuzuia

Hali hii huzuiwa kwa kula vyakula vyenye nyunzinyuzi za kutosha kama vile

matunda na mbogamboga, kunywa maji ya kutosha na kufanya mazoezi mara

kwa mara

42. Kuvimbiwa

Ni hali ambayo mfuko wat umbo hujaa, kuwa mgumu au kuvimba, mara nyingi

hutokanana na mkusanyiko wa gesi katika mfuko wat umbo. Tatizo la

kuvimbiwa husababishwa na kula chakula kingi kupita kiasi , kula vyakula

vinavyosababisha gesi au tumbo kutovumilia baadhi ya vyakula

Dalili za mtu kuvimbiwa nit umbo kuuma, kuhisi tumbo kujaa gesi na kupiga

mbweu.wakati mwingine gesi hiyo huwa na harufu kali na mbaya

Njia za kuzuia

Ili kuzuia unapaswa kula chakula kwa kiasi na kutafuna polepole ili kupunguza

kiasi cha hewa inayomezwa. Vilevile, kunywa maji ya kutosha ili kurahisisha

mmeng’enyo wa chakula katika mfuko wat umbo. Kupunguza ulaji wa vyakula

vyenye gesi kama vile maharage na unywaji wa vinywaji vyenye gesi kama vile

sod. Pia, ulaji wa matunda na mboga za majani huzuia kuvimbiwa

3. Kiungulia

Ni hali ya kuhisi moto au maumivu kifuani au kooni yanayosababishwa na aside

ya tumbo kupanda juu, hali inayochangiwa na kula vyakula vyenye mafuta au

viwango vikali, kula sana kisha kulala Pamoja na kunywa pombe au kahawa

nyingi

Njia za kuzuia

Unaweza kuzuia kiungulia kwa kula chakula taratibu ili kurahisisha

mmmeng’enyo wa chakula. Pia kula chakula kidogokidogo lakini mara kwa

mara pia kupunguza viungo na mafuta mengi.Epuka kulala mara tu baada ya

kumaliza kula.Vilevile epuka kufanya mazoezi au kazi ngumu muda mfupi

baada ya kula chakula. Hali ya kiungulia ikizidi ni vyema kupata ushauri wa

kitabibu

fano wa pili, kitendo kinarudiwa mpaka jambo fulani litokee (kihusika kiguse

ukingo) kwenye mfano wa tatu kitendo kinarudiwa bila kikomo hadi mchezo

uishe

5BACK TO SCHOOL ONLINE MATERIAL

Karibu ujipatie

1.scheme of work| – azimio la kazi

2.Lesson plan – Andalio la somo

3.Lesson Notes – Nukuu za somo

4.Log Book – Shajara

5.Holiday Package

Karibu kwa huduma nzuri uaminifu na uhakika Zaidi

Piga 0694361925 WhatsApp 0627064154

67891011121314151617………..………………………. THE END ……………………………

18

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *