January 12, 2026

WatuCrash

📚 Education & Learning Hub (Primary + Secondary)

ca-app-pub-5779332594648854/1423561520
Kiswahili

NUKUU ZA SOMO LA KISWAHILI 2025 DARASA LA NNE

ZABIKHA ISLAMIC NURSERY AND PRIMARY SCHOOL

NUKUU ZA SOMO LA KISWAHILI 2025 DARASA LA NNE

11.0 KUWASILIANA KATIKA MIKTADHA MBALIMBALI

1.1 Kuendeleza mazungumzo katka miktadha mbalimbali.

a) Kulinganisha vitu kwa kutumia maneno [kuliko,Zaidi ya ,kama mithili

ya na mfano wa] katika miktadha mbalimbali

i. Kujenga dhana ya ulinganishi

Ulinganishi ni hali ya kuwa sawa

Ukubwa na udogo wa kitu ni mwonekano wake unaotokana na

umbo lake au eneo lake.

– Kutaja majina ya vitu mbalimbali vinavyopatikana katika

mazingira;Kiti,meza,kitanda,sahani,kijiko,upawa,mwiko,milima,

magari,

Magari,pikipiki, tikiti,dirisha,simu,mnazi,gauni,nyumba,ghorofa

na kitana.

ii. Kulinganisha vitu mbalimbali kwa kutumia maneno [kuliko,Zaidi

ya,kama mithili ya na mfano wa]

Ifuatayo ni mifano mingine ya ulinganishi:

1. Kiatu kile ni kikubwa Zaidi ya hiki

2. Chumba change ni kikubwa kuliko

3. Mlango ule ni mkubwa Zaidi ya huu

4. Dada yangu ni mdogo kuliko dada yako

5. Shamba hilini dogo kuliko lile

6. Kalamu hii ni ndogo Zaidi ya ile

7. Kitabu chetu ni kidogo kuliko kitabu chao

8. Upana wa shule yetu ni kama wa shule yenu

9. Ukubwa wa Dar es Salam si sawa na wa Dodoma

10. Rangi ya viatu si sawa na rangi ya viatu vyangu

2Tunatumia maneno kama vile kama na sawa na kulinganisha

Ukubwa na Udogo wa vitu vinavyofanana.

Mfano:

1. Mtoto huyu ni mdogo kama sungura

2. Ukubwa wa gari lao ni sawa na wa gari letu

3. Shamba langu ni dogo kama lile la mjomba

4. Shangazi yangu ni mrefu kama mjomba

5. Unene wa kiatu hiki ni sawa na wa kile pale

Zoezi 1

Jibu maswali yafuatayo sahihi

1. Andika kweli kwa kauli ambayo ni sahihi na Si kweli kwa

kauli ambayo si sahihi

a) Mji wa Zubeda ni mdogo kuliko wa Sara

b) Mji wa Sara una barabara chache kuliko mji wa

Zubeda

c) Miji yote miwili ina idadi sawa ya watu

d) Sara alitembelewa na Zubeda

2. Tunga sentensi sahihi kwa kutumia maneno yafuatayo

ya ulunganishi:

a) Kama

b) Sawa na

c) Kuliko

d) Zaidi ya

e) Mithili

32. kutumia miundo Chora picha za michoro ifuatayo kisha linganisha kwa

( Sawa na ,kuliko, kama na Zaidi ya )

a. Kikombe

b. Gauni

c. Chupa

d. .Dirisha

b ) Kusimulia matukio kwa kuzingatia njeo za wakati ; uliopo[-na-

],uliopita[-li-],ujao ta,[- -],mazoea,[-hu-] na hali timilifu [-me-]

i. Kueleza matukio kwa kutumia nyakati mbalimbali katika

sentensi.

– Kutaja nyakati mbalimbali za utendaji

Wakati ni nini?

Wakati ni muda unaoashiria tendo au tukio Fulani lililofanyika au

linavyofanyika na litakavyofanyika.

– Nyakati zimegawanyika katika sehemu kuu tano

a. Wakati uliopita [LI]

b. Wakati uliopo [NA]

c. Wakati ujao [ TA]

d. Wakati mtimilifu [ ME]

e. Wakati wa mazoea [HU]

i. Kueleza matukio mbalimbali kwa kutumia nyakati anazojifunza

4Wakati uliopo [NA]

Wakati uliopo ni muda unaoashiria kuwa tendo linaendelea

kutendeka.

Mfano;

1. Wanafunzi wanasoma darasani

2. Sisi tunalima bustani

3. Nyinyi mnaoga bafuni

4. Wageni wanaingia ndani

5. Yeye anaimba taratibu

6. Unakula ugali na kitoweo gani?

7. Mjomba anapalilia shamba

8. Mnatembeataratibu sana

9. Wao wanapigana ngumi

10. Mama anaswali asubuhi

Wakati ujao [TA]

Wakati ujao ni muda unaoashiria kuwa tendo litafanyika badae.

Mfano;

1. Wanafunzi watafunga shule mwezi ujao

2. Walimu wataandika kitabu kizima

3. Sisi tutakula chakula kizuri

4. Watapalilia shamba lao

5. Yeye hataondoka mpaka amalize kazi

6. Mtakimbia wapi?

7. Yeye ataswali adhuhuri

8. Sisi tutampiga hadi afe

9. Tutaandika kama tulivyoelekezwa

5Wakati uliopita [LI]

Wakati uliopita ni muda unaoashiria kuwa jambo /tendo lilitendeka muda

mrefu uliopita

Mfano;

1. Alinunua debe la senene jana

2. Mgonjwa alipelekwa hospitali

3. Tulikula wali na tulikunywa maji

4. Walichimba kisima kirefu

5. Wao waliimba wimbo mzuri

6. Muliingia ukumbini saa ngapi?

7. Mwalimu aliingia darasani

8. Mwanafunzi aliandika somo

9. Mimi nilisoma kitabu cha kiswahili

Wakati mtimilifu [ME]

Wakati mtimilifu ni wakati unaoashiria tendo limefanyika punde tu [sio

muda mrefu]

Mfano;

1. Ameondoka leo asubuhi

2. Wameingia madarasani

3. Amekula chakula chote

4. Tumesoma dua leo asubuhi

5. Wao wamebeba madawati

6. Mwalimu amewaadhibu wanafunzi wakorofi

7. Wale wmegombana

8. Asha amejifungua leo asubuhi

69. Sisi tumekunywa kahawa

Zoezi 1

Andika sentensi hizi katika wakati mtimilifu

1. Wanafunzi walifanya mgomo

2. Baba ataezeka nyumba

3. Daktari analing`oa jino

4. Nitaandika waraka mpya kwa baba yangu

5. Wale wamegombana

Andika sentensi katika uliopo

1. Vyura hao waliishi kwenye miji miwili

2. Walisalimiana katika safari

3. Mji wa kaskazini ulikuwa mbali na wa kusini

4. Baba alirudi jana jioni

5. Wote walipanda juu

Wakati wa mazoea [ HU]

Wakati wa mazoea ni wakati unaoanesha huwa kkitendo hufanyika kila

siku na mara kwa mara kitendo hicho hufanyika.

Soma kifungu cha habari kifuatacho kwa usahihi

Sifa za mbweha

Mbweha nu mnyama mdogo wa porini anayefanana na mbwa. Ana

mdomo uliochongoka ,maskio yaliyosimama na mkia weny manyoya

mengi.

Mbweha huishi kwenye vichaka .Mnyama huyu huwinda na kutafuta

chakula chake usiku. Maana yake ni kuwa mbweha hulala wakati wa

mchana . Anapowinda , hurukia mawindo yake kama wafanyavyo

7paka.Mbweha hula wanyama kama vile sungura,mijusi na panya .Vilevile

,hula wadudu mbalimbali na hata matunda.Mnyama huyu huweza

kupanda hata juu ya miti..

Mbweha huzaa mara moja kwa mwaka huweza kuzaa watoto hadi

kumi .Mbweha anapozaa ,Jike hukaa na watoto na dume huenda

kuwinda na kuleta chakula .Masikio ya mbweha husikia panya wakiwa

wanachimba chini aridhini.

Hakika yapo mambo mengi ya kuvutia yanayomhusu mnyama huyu

mbweha.

Zoezi 2

Badili sentensi zifuatazo kuwa katika hali mazoea

1. Mimi numepiga mswaki asubuhi

2. Sisi tunacheza mpira jioni

3. Nyinyi mnaenda kulima

4. Yule amesoma vitabu vya hadithi

5. Wao wamefaulu somo la hisabati

6. Nuru na Chitola wamefanya maigizo

Zoezi la 3

Chagua neno sahihi kwenye kisanduku ili kukamilisha sentensi.

Akajichubua,nguzo,mabuyu,matunda,kivuli,madawati

1. Matunda ya mbuyu yanaitwa _______________

2. Wakati wa jua kali tunakaa kwenye ___________

83. Nyumba nyingi kijijini zimejengwa kwa __________

4. Maji ya ___________ ni matamu sana

5. Wanafunzi darasani wanakalia ____________

6. Alijikwaruza kwa jiwe _______________ ngozi yake

iii. Kukanusha matukio ya nyakati mbalimbali kwa kutumia sentensi.

a) Kueleza maana ya ukanushi

Ukanushi ni nini ?

Ukanushi ni tendo la kupinga au kukataa jambo Fulani .

Tunapokanusha sentensi tunadondosha baadhi ya silabi katika kitenzi au

tunabadili na kuongeza baadhi ya silsbi lakini hatubadili maana ya msingi

ya neno.

Mfano : 1

KUPATA NOTES KAMILI WASILIANA NASI

0675701982/0743441251/0679241251

 NOTES

 LESSON PLAN

 EXAMS

 SCHOOL ACTION PLAN

9

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *